Majogoo wa jiji Liverpool wameendelea kuifukuzia Manchester City kileleni baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Leicester City mchezo wa ligi kuu England uliochezwa Alhamisi usiku uwanja wa Anfileld.

 


 

Magoli  ya Mreno, Diogo Jota dakika ya 34 na 87 na kufikisha pointi 51 baada kucheza mechi 23, ikiwa katika nafasi ya pili, ikizidiwa pointi tisa na mabingwa watetezi, Manchester City ambao pia wamecheza mechi moja zaidi.

 


Leicester City inabaki kwenye nafasi ya 12 na pointi zake 26 baada ya  mechi 21.