Manchester City imeendeleza ubabe kwenye ligi kuu ya England baada ya kuichapa Brentford kwa mabao 2-0 mchezo uliochezwa jana usiku kwenye uwanja wa Etihad, Manchester.

 


City walipata magoli yao kupitia kwa mchezaji wa kimataifa wa Algeria Riyad Mahrez kwa mkwaju wa penati baada ya Rahim Sterling kuchezewa faulo ndani ya 18.

 

Vijana wa Pep Guardiola waliongezaa bao la pili na kujihakikishia alama tatu kupitia Kevin de Bruyne, city wanaongoza ligi hiyo wakiwa na alama kwa tofauti ya pointi 12, wakiongoza kwa alama 60 wakiwaacha Liverpool kwenye nafasi ya pili na alama 48.

Matokeo ya michezo mingine ya Epl iliyochezwa jana ni kama ifuatavyo👇👇👇