Senegal imetinga hatua ya fainali ya michuano ya Afcon bada ya kuishushia kipigo timu ya taifa ya Burkina Faso cha mbao 3-1  kwenye mchezo wa nusu fainali uliopigwa jana usiku katika dimba  la Ahmadou Ahidjo, Yaounde Cameroon.




Abdou Diallo alianza kufungua akaunti ya mabao baada ya kuiandikia Senegal bao la kuongoza dakika ya 70,dakika sita baadaye Idrissa Guaye anayekipiga PSG ya Ufaransa, akakwamwisha mpira wavuni  akimalizia pasi safi ya Sadio Mane nakuandika bao la pili kwa Senegal.

 

Burkina Faso wakaamka na kufanikiwa kupata bao dakika ya 82 kupitia kwa Blati Toure na kufanya matokeo kuwa 2-1.


Nyota wa Liverpool  Mane ndiye aliyezima ndoto za Burkina Faso za kwenda fainali baada ya kuweka kimiani bao la tatu kunako dakika ya 87 ya mchezo.

 

Hii ni fainali ya tatu kwa Senegal wakiwafanya hivyo mwaka 2002, 2019 ambazo zote walipoteza, mshindi wa mechi ya leo kati ya mwenyeji Cameroon dhidi ya  Misri atacheza na Simba wa Terenga kwenye mchezo wa fainali jumapili.