Shirikisho la soka Afrika CAF  limeruhusu mashabiki 35,000 kuhudhuria mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika kati ya Simba dhidi ya ASEC Mimosas mchezo ukataochezwa  jumapili Februari 13, kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.

 


Akitoa taarifa hiyo leo Februari 1, meneja wa Habari na Mawasilino wa klabu hiyo Ahmed Ally amesema waliomba kupatiwa idadi kubwa zaidi ya mashabiki lakini  mamlaka husika wamruhusu  idadi hiyo ya mashabiki.

 

Aidha mashabiki wamekubushwa kuchukua tahadhari zote za Covid 19, ikiwemo kutakasa mikono kuvaa barokoa,  kukaa kwa nafasi kwa mashabiki watakaingia uwanjani (social distance) na siku ya mchezo tiketi hazitauzwa uwanjani.