Rais wa heshima wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’ Februari 9,  amekutana na kuzungumza na wachezaji na benchi la ufundi la tomu hiyo kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosa ya Ivory Coast.





Akizungumza Azam Tv mara baada ya kikao hicho Dewji amesema  malengo makuu ni kufanya vizuri kwenye michuano hiyo baada ya kutolewa kwenye ligi ya mabingwa.


“Tunahitaji ubingwa na mafanikio ya kimataifa, maana hata mimi licha ya kupata hasara katika uendeshaji wa klabu bado naendelea kutoa fedha na ninyi nataka mkajitume”

 

Mashabiki wa Simba ni wa muhimu sana kwa maendeleo ya klabu yetu, natangaza kupunguza viingilio na Jumapili mzunguko itakuwa elfu 3 ili wote waweze kuitazama timu yao" Mo Dewji.

 

Simba itawavaa ASEC Mimosas ya Ivory Coast Jumapili kuanzia Saa 10:00 jioni Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.