Mwimbaji nyota wa muziki  wa Rnb  Robyn Rihanna Fenty maarufu kama Rihanna na mpenzi wake msanii wa Hip Hop  Rakim Mayers maaruf kama A$AP Rocky wanatarajia mtoto wao wa kwanza wakiwa pamoja, wapenzi hao walithibitisha kwenye picha zilizopatikana na kwenye mtandao wa E! News.

 


Katika picha hizo, zilizopigwa jijini New York mwishoni mwa wiki na kuchapishwa Jumatatu, Januari 31, Rihanna anaonekana akionesha tumbo lake huku A$AP akimbusu paji la uso.

Habari hii ya ujauzito inakuja miaka miwili baada ya kuwa marafiki wa muda mrefu huku wakihusishwa na taarifa kuwa ni wapenzi, tetesi zilizokuwepo muda mfupi baada ya kutengana na Hassan Jameel.


Uhusiano ulianza baada ya nyota hao kuonekana wakiwa pamoja huko New York.