Ikiwa zimepita siku mbili tangu timu ya taifa ya Misri ipoteze  mchezo wa fainali dhidi ya Senegal, staa wa Liverpool Mohamed Salah ameanza mazoezi leo Februari 8, kujiwinda na michezo ya ligi kuu England.

 


Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesema kuna uwezakano mkubwa wa  Salah kucheza katika mchezo wa Epl dhidi ya Leicester City Alhamisi, kuhusu Mane, Klopp amesema uwezakano wa kucheza haupo maana bado hajaripoti kambini.


Salah  hakupiga mkwaju ya penati kwenye mchezo wa fanaili  jumapili ambayo walipoteza huku Mane akipiga  Penati ya ushindi kwa Senegal.