Ni Simba dhidi ya Tanzania Prisons leo Februari 3, mechi ya Ligi kuu NBC ambayo huwa inavuta hisia za wapanda kandanda hapa nchini.

 


Msimu uliopita wajela jela walifanikiwa kuondoka na alama nne mbele ya Simba wakishinda na kutoa droo japo Simba alibeba ndoo ya ligi kuu.

 

Wote wametoka kupoteza michezo yao ya mwisho na hata ubora wao msimu huu unaonekana kidogo kushuka na kuifanya mechi ya leo kuzidi kuwa ngumu.


Simba wametoka kupoteza michezo miwili ya Ligi Kuu, leo hii watataka kutafuta alama tatu ili kupunguza alama kati yake na anayeongoza msimamo wa Ligi.



Tanzania Prison wakiwa wanashika mkia kwenye msimamo nao wanatafuta alama tatu muhimu kwao kujikwamua sehemu waliopo wakiwa alama 11 baada ya kushuka dimbani mara 13, imepoteza michezo nane na ina sare mbili.



Simba watataka kurudisha ari ya ushindi ili wachezaji warudishe hali ya kujiamini kwenye kikosi chao kabla ya mchezo wa kombe la shirikisho.

Majibu ni leo saa 1:00 usiku katika dimba la Benjamin Mkapa.