Bingwa mtetezi
wa ligi kuu ya NBC Simba,
Goli pekee
la Simba limefungwa kwa mkwaju wa penati na mshambuliaji Meddie Kagere dakika ya
67 baada ya beki wa Prisons kuunawa mpira ndani ya 18.
Simba ambayo
ilianza viungo wengi iliafanikiwa kumiliki mpira ambao haukuwa na madhara
kwenye lango la Prisons ambao waliamua kupaki basi na kucheza mpira ya
kushtukiza ambayo ilionekana kuwa ya hatari langoni mwa Simba.
Iliwachukua Simba dakika 67, kupiga mpira uliolenga lango (shot on target) ambao ni mkwaju wa penati ya
Kagere.
Baada ya
mchezo kocha msaidizi wa wekundu wa msimbazi Suleman Matola, amesema hajaridhika
na ushindi kiduchu walioupata lakini amekiri ni nguma kucheza na timu kama
Prisons ambayo muda mwingi wanazuia.
Mnyama Simba amefikisha alama 28 baada ya michezo 14, Yanga inaongoza msimamo wa ligi na alama 35.
0 Maoni