Bingwa mtetezi wa  kombe la Azam Sports Federation Cup Simba imefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kibabe baada ya kuibuka na ushindi wa mzito wa mabao 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting, mechi iliyochezwa leo usiku Februari 16 uwanja wa Benjamin Mkapa Dar.




Katika mchezo nyota wa Kimataifa wa Zambia Cloutus Chmama ameondoka na mpira baada ya kufunga magoli matatu Hat Trick akifunga kwenye dakika ya 25’ 28 na 75, huku mshambuliaji Rafael Bocco akifunga mabao mawili dakika ya 2 na 40.

 

Beki wa Ruvu Shooting aliwazadia bao Sib baada ya kujifunga katika kipindi cha kwanza dakika ya 44 ya mchezo, Jimmyson Mwanauke naye akitokea benchi aliiandikia simba bao dakika ya 70 .