Vinara wa Ligi kuu Yanga wanashuka dimbani leo Februaru 5 majira ya saa 1:00 usiku uwanja wa Benjamin Mkapa kuwakaribisha Mbeya City.

 


Yanga ambayo haijawahi kupoteza mchezo dhidi ya Mbeya City katika misimu minne mfululizo iliyopita tangu mwaka 2017, ikishinda mara nne na kutoka sare mara nne.

 

Wananchi wanakutana na Mbeya City ya tofauti ikiwa ikiwa imejikusanyia alama 22, imepoteza mchezo mmoja kati 13   walipoteza  dhidi ya Coastal Union walifungwa mabao 3-2 na ina sare saba.

 

Licha ya kufunga magoli 17 lakini safu ya ulinzi imeruhusu magoli 11 na leo Mbeya City watakuwa na kibarau kigumu cha kuizua  safu bora ya ushambuliaji msimu Yanga imetikisa wavu wa wapinzani mara 23.


Je Mbeya City watafanikiwa kuizua  Yanga ambayo iko kwenye kiwango bora kwa sasa wakiwa na safu ya ushambuliaji hatari ikiongozwa na Fiston Mayele? Majibu ni saa 1:00 Usiku.