Vinara wa ligi kuu ya NBC,Yanga ikiwa katika dimba la nyumbani Benjamin Mkapa leo Februari 5, imelazimishwa Suluhu na Mbeya City hii ni ya tatu  msimu huu kwenye mechi za Ligi.

 


Mbinu za Mbeya City kocha Mathias Lule zimeonekana kuwasumbua Yanga katika akiafanikiwa kuibana Yanga eneo kiungo na kuwafanya Khalid Aucho Gift Mauya kushindwa kucheza kwa UUhuru

 

Uimara wa mlinda mlango wa Mbeya City Deogratis Munisgi ‘Dida’ umeunyima ushindi Yanga baada ya kuokoa mpira wa Chiko ushindi dakika za lala salama.

 

Yanga imeendelea kubaki kileleni na alama 36 huku Simba amabayo inshuka dimbani kesho ina alama 28 na kama watashinda watapunguza alama na kubaki tano.