Nyota wa Kimataifa wa Morocco Hakim Ziyech ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa hiyo baada ya kutoa kwa mgogoro  na kocha Vahid Halilhodzic.

 


Halilhodzic hakumjumuisha Ziyech kwenye kikosi kilichoshiriki michuano ya AFCON iliyomalizika Jumapili hii nchini Cameroon.

 

Staa huyo wa Chelsea alituhumiwa kocha wake kuwa  alidanganya kuwa ni majeruhi ili asicheze timu ya taifa, mara ya mwisho kuitwa kwenye kikosi cha Simba wa  Atlas ilikuwa June 2021.

Akiwa Abu Dhabi Falme za Kiarabu akijiandaa na mechi za Klabu Bingwa ya Dunia akiwa na klabu ya  Chelsea Ziyech amesema anajua kuwa uamuzi wake utawaumiza mashabiki  lakini budi  kuchukua maamuzi hayo.