Mabingwa wa watetezi wa ligi kuu ya NBC Simba jana usuku ilifanikiwa kuondoka na alama tatu dhidi ya Dodoma Jiji, baada ya kuichapa kwa mabao 2-0 mchezo uliochezwa kwenye uwanja Benjamin Mkapa Dar es salaam.
| Kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama Akishangilia baada ya kufunga goli la kuongoza dhidi ya Dodoma Jiji. |
Magoli
ya Simba yalifungwa Clatous Chama dakika ya 57 kwa makwaju wa penalti na
kumfanya sasa kufikisha magoli matatu akicheza mechi sita tangu arejee tena
Msimbazi.
Goli
la pili lilizamishwa na mshambuliaji Meddie Kagere dakika ya 75’ akiunganisha
vema krosi ya Peter Banda, Kagere sasa anafikisha magoli 6 kwenye ligi ya NBC.
| Rally Bwalya akimpongeza Meddie Kagere baada ya kukamisha bao la pili dhidi ya Dodoma Jiji |
Kwa
matokeo ya Jana Simba sasa imefikisha pointi 37 baada ya kushuka dimbani mara
17, Yanga inaongoza ligi hiyo kwa alama 45.
0 Maoni