Klabu ya Chelsea ya England imepanga kuanza mazungumzo na kocha wa zamani wa Barcelona na Timu ya Taifa ya Hispania Luis Enrique.

Enrique amesafiri leo kuelekea jijini London Uingereza kwa ajili ya mazungumzo na 'The Blues' ili aweze kuwa Kocha wa klabu hiyo.

                                       Kocha wa zamani wa Barcelona Luis Enrique

Hivi karibuni Chelsea walimfukuza kazi kocha Graham Potter baada ya kuwa na mfululizo wa matokeo mabaya kwenye ligi kuu ya England na Ligi ya Mabingwa Ulaya.

The blues pia wanahusishwa na  Julian Nagelsmann ambaye wiki iliyopita alifukuzwa kazi katika kalbu ya Bayern Munich ya Ujerumani.